Seli

Seli za ngozi ya mtu chini ya hadubini.

Seli (kutoka Kilatini cellula = chumba kidogo) ni chumba kidogo ndani ya mwili wa binadamu, wanyama. mimea n.k.

Mwili wote wa kila kiumbehai hufanywa kwa seli. Viumbehai vidogo sana kama bakteria huwa na seli moja tu. Mwili wa mwanadamu huwa na seli trilioni 100 au 1014.

Kila yai ni seli moja tu, hivyo seli kubwa duniani ni yai la mbuni.

Seli za kawaida ni ndogo sana kiasi kwamba huweza kutazamwa tu kwa kutumia hadubini.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy