Simba

Kwa kundinyota inayoweza kuitwa "Simba" angalia hapa Asadi (kundinyota)

Simba

Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Carnivora (Wanyama mbua)
Nusuoda: Feliformia (Wanyama kama paka)
Familia: Felidae (Wanyama walio na mnasaba na paka)
Nusufamilia: Pantherinae (Wanyama wanaofanana na chui)
Jenasi: Panthera
Spishi: P. leo
(Linnaeus, 1758)
Ngazi za chini

Nususpishi 2:

Msambao wa simba
Msambao wa simba

Simba (jina la kisayansi: Panthera leo[1]; kwa Kiingereza lion) ni mnyama mkubwa mla nyama (carnivore) wa familia ya Paka[2] katika ngeli ya mamalia. Maana yake ni kwamba simba hufanana na paka mkubwa.

Siku hizi simba wako hasa Afrika kusini kwa Sahara.

Simba wa Asia walipatikana zamani kati ya Uturuki na Bangladesh lakini ni wanyama 300 pekee waliobaki katika hifadhi ya wanyama huko Gujarat nchini Uhindi.

Nususpishi nyingine zilikuwepo Ulaya na pia Afrika ya kaskazini lakini zote zimekwisha kwa sababu waliwindwa vikali.

Chakula chao ni nyama inayopatikana kwa kuwinda wanyama. Tofauti na paka wengine, simba huishi na kuwinda katika vikundi vyenye wanyama 10-20. Kila kundi lina eneo lake na kuitetea dhidi ya simba wengine. simba jike ndiye anayewinda na baada ya kumkamata mnyama, dume ndiye anayeanza kula na hasa uanza kula viu vya ndani kama vile utumbo, maini, ndipo jike na watoto wanafuata kwa kula.

Dume anafikia urefu wa mwili pamoja na kichwa wa sentimita 170 hadi 250; kimo cha mabegani ni cm 120. Dume mkubwa anaweza kuwa na uzito wa kilogramu 225. Jike ni mdogo wake akiwa na urefu wa 140 hadi 175 cm, kimo cha mabegani cha cm 100 na uzito wa kg 150.

Dume anatofautishwa kirahisi kutokana na Nywele refu za shingoni ilhali jike hana.

Jike anaanza kuzaa akifikia umri wa miaka 2-3. Baada ya kubeba mimba kwa miezi 3 1/2 anazaa wadogo 2-3. Wakati mwingine idadi hii inaweza kuwa hadi wadogo 6 lakini wanaozidi 3 kwa kawaida wanakufa mapema.

  1. jenasi Panthera inajumuisha na wanyama wengine ikiwemo tiger wa bara la Asia, chui na puma
  2. hii familia inajumuhisha paka wote wanaopatikana duniani, wakiwemo wanaofugwa nyumbani, paka pori, tiger, simba, chui na wengineo.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy