Tanganyika

Bendera ya koloni ya Tanganyika.
Bendera ya Tanganyika tangu 1961 hadi 1964.
Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Tanganyika ni jina la kihistoria la sehemu kubwa ya Tanzania ya leo, yaani ile yote isiyo chini ya serikali ya Zanzibar.

Kwa sababu za kisiasa, mara nyingi huitwa "Tanzania bara" ingawa ina visiwa pia, hasa Mafia na Kilwa.

Tanganyika ilikuwa sehemu kubwa ya koloni la Ujerumani hadi vita kuu ya kwanza ya Dunia. Baada ya mwaka 1916 ilivamiwa na Uingereza na Ubelgiji. Kuanzia mwaka 1922 Tanganyika ilikuwa eneo la kudhaminiwa kwa niaba ya Shirikisho la Mataifa lililokuwa chini ya Uingereza ikawa nchi huru kati ya miaka 1961 - 1964, mwaka wa kwanza kama ufalme, halafu kama jamhuri.

Mwaka 1964 iliungana na Zanzibar na kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy