Ukulu mtakatifu au Ukulu wa Kitume (kwa Kiingereza: Holy See au Apostolic See) kwa maana asili ni kiti maalumu alichowekewa Papa katika Kanisa kuu la Roma, ambacho ni ishara ya mamlaka ya kiaskofu ambayo Wakatoliki wanasadiki anayo ya kufundisha, kutakasa na kuongoza Taifa la Mungu kokote duniani.