Upumuo

Video ya mnyama wa kike jamii ya mamba akipumua.

Upumuo ni kitendo cha kuvuta hewa ndani ya mapafu au oksijeni kupitia viungo vingine kama vile matamvua ya samaki, halafu kutoa gesi ya CO2 pamoja na hewa iliyotumiwa.

Kuna pia upumuo wa ndani ambayo ni kazi ya seli za mwili kupokea oksijeni na kuitumia kwa mchakato wa oksidisho ndani yao.

Kazi ya mapafu katika upumuo
(Njia ya hewa inaanza mdomoni na puani ; musuli za kiwambo tumboni (njano-nyekundu) zinajikaza au kulegeza na hivyo kupanua au kupunguza ukubwa wa mapafu (bluluu nyeupe/zambarau)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy