Wakalenjin

Pokot-Frauen.

Wakalenjin ni kundi la makabila ya magharibi mwa Kenya, hasa katika uliokuwa mkoa wa Bonde la Ufa, wanaoongea lugha za Kiniloti zilizo karibu. Wasemaji wa lugha hizo wako pia Tanzania na Uganda.

Kati ya vikundi hivi ni Waelgeyo, Wakipsigis, Wamarakwet, Wanandi, Wasabaot, Waterik na Watugen. Mababu wao walihamia Kenya kutoka Sudani karne nyingi zilizopita na wengine wanakadiria wamefika tayari tangu miaka 2,000.

Wakati mwingine hata Wapokot wanahesabiwa kati ya Wakalenjin lakini kwa kawaida wanajitazama kama kundi la pekee hata kama lugha yao ni ya karibu.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy